THE POWER OF STORY TELLING IN MUSIC SESSION TWO.. - a podcast by martine

from 2020-08-06T03:00

:: ::

Kwenye Episode hii Tumeongelea Nyimbo ambazo wasnii Nguli watatu wameweza kutumia adithi zenye ujumbe mzito na kuweza kuziweka kwenye Ngoma, Kwa namna nyingine Tunaweza kusema wasanii hawa wametumia simulizi ambazo zipo mtaani wa watu wanakumbana nazo kwenye maisha ya kawaida na wao wakaamua kuzitumiakatika Sanaa ya muziki na utunzi wenye mpangilio, hatimaye na wakatuletea ngoma au mziki unao ishi siku zote.


Kwenye part Hii ya Pili, Utaweza kusikia Namna ambavyo msanii Ferooz alivyoweza kuakisi na kusimulia Ugonjwa wa ukimwi na kuweza kuelezea na kufundisha jamii, madhara ya UKIMWI, Pia na kuweza kusambaza elimu kubwa ambayo ilikuwa Haijawafikia wengi san asana kwenye Taifa letu la Tanzania.


Tumeenda mbali Zaidi na kuona Mafanikio ya ngoma hii ambayo Feroozi alishirikiana na Professor Jay na kuweza kuacha Harama kwenye ulimwengu wa Muziki unao tumia simulizi na adithi kufikisha ujumbe.


Pia kwenye episode hii Utapata Kujua wimbo wa nikusaidieje wa Professor Jay pia ulivyotumia nguvu ya adithi na kuleta mapinduzi makubwa ya kifikira kwa wanaume, ya kwamba mwanamke bora anapatikana kijijini wala sio mjini na mambo mengine mengi.


Tumeweza kwenda mbali Zaidi na kuangalia wimbo wa msanii Diamond Platinum Wimbo wa Je Utanipenda, wimbo ambao umepata mafanikio makubwa kutokana nakile alichoweza kuakisi msanii Diamond, sana sana Kwenye upande wa kipato cha mwanaume Pale inapotokea Kutetelekakwenye uchumi na mambo kutokwenda sawa.


Kwa yote haya yameweza kuelezea na kuonesha nguvu ya adithi kwenye muziki, Endapo ikitumika na kuelezewa kwa ufasaa kabisa na Mwanamuziki au mwanafasii anaye ilisha jamii jambo la kusikika na kuweza kuleta mabadiriko.



---

Send in a voice message: https://anchor.fm/martine945/message

Further episodes of NMU PODCAST

Further podcasts by martine

Website of martine